Akiwa angani: Obama akitazama mechi ya mwisho ya Marekani dhidi ya Ujerumani akiwa kwenye ndege yake.
RAIS wa Marekani, Barack Obama ameonesha jinsi gani kombe la dunia ni muhimu kwa taifa lake baada ya kuamua katazama mchezo wa mwisho wa kundi G dhidi ya Ujerumani akiwa kwenye ndege yake binafsi.
Obama alikuwa anasafiri kwa ndege kutoka Maryland kwenda Minnesota wakati Marekani ikicheza mchezo muhimu na alihakikisha hakosi mchezo huo kupitia matangazo ya moja kwa moja kwenye luninga iliyopo kwenye ndege yake.
No comments:
Post a Comment