Friday, August 8, 2014
On 1:23 AM by Unknown No comments
Tumezoea kusikia wakati wa kufunga ndoa watu wakila kiapo kuwa watapendana hadi kifo kitakapowakuta, kiapo ambacho kwa baadhi ya watu huwa kama neno lililozoeleka kwenye shughuli ya harusi na baadae wakavurugana bila kulijali neno hilo.
Hii ni tofauti kwa Don na Maxine Simpson, wanandoa waliokuwa wakiishi katika jimbo la Bakersfield, California nchini Marekani ambao wameweka historia ya kushangaza walipopoteza maisha kwa pamoja baada ya kuishi katika ndoa kwa miaka 62 bila kuachana wala kutengana.
Kwa mujibu wa BBC, wanandoa hao walikuwa wamelazwa hospitalini kwa sababu ya hali duni ya afya iliyotokana na umri wao mkubwa. Inaelezwa kuwa wanandoa hao waliaga dunia saa nne baada ya kushikana mikono na kuahidiana kuwa wataendelea kupendana hata kifo kitakapowakuta.
Don na Maxine wakiwa hospitalini
Muda mfupi baada ya Maxine kufariki na mwili wake kuondolewa katika chumba walichokuwa wamelazwa pamoja, mumewe Don alifariki pia saa nne baadae kutokana na uchungu mkubwa na mshituko wa kuondokewa na mpenzi wake.
Mjukuu wake aliyetajwa kwa jina la Melissa Sloan, aliiambia KERO-TV kuwa babu yake alimpenda sana Maxine tangu walipokutana mwaka 1952 akiwa bindi mdogo katika mashindano ya Bowling.
“Babu yangu alikuwa anatamani kuishi na nyanya yangu na hata baada ya wawili hao kuanza kuugua kutokana na umri wao mkubwa waliwaomba wasimamizi wa hospitali walimolazwa wasiwatenge.” Alisema Mellisa.
Hadi mauti ilipowafika, Don aliwakuwa na umri wa miaka 90 na mkewe alikuwa na miaka umri wa miaka 87.
Don na Maxine walipokutana 1952
Kama watu hukutana ahera na maisha yakaendelea kama kawaida, wawili hao bila shaka watayaamishia mapenzi yao ahera penye amani ya kudumu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Slider
MusicView All
TechnologyView All
PicturesView All
GamesView All
Labels
Category
Ads
Text
Find Us On Facebook
Link List
Contact Form
Blogroll
Flickr Images
728x90 AdSpace
Label
FashionView All
Latest News
Popular Posts
-
It's good to be Iron Man — Robert Downey Jr. once again leads Fo...
-
Tumezoea kusikia wakati wa kufunga ndoa watu wakila kiapo kuwa watapendana hadi kifo kitakapowakuta, kia...
-
Brad Pitt and Angelina Jolie will finally tie the knot, only for a movie. According to a scoop from The Hollywoo...
-
Brad Pitt has owned a gun since he was very young. In a new interview with Radio Times to promote his new flick " Fury ", the a...
-
Will Smith , who is gearing up for his new film " Focus " with Margot Robbie , opens up about his experience in 25 y...
-
Miley Cyrus updated her Instagram with lots of photoshopped pictures. This time, Justin Bieber 's Calvin Kl...
-
Sio Wakati Wote Ni Wa Kazi Hata Kmaa Ni Mtu Maarufu Kuna Muda Unatakiwa Kukutana Na Watu Tofauti Na Kujipa Raha kwa Nafasi Kama Unavyomuo...
-
Channel O walitisha sana na maandalizi ya mwaka huu wa 2014 ambapo magari mbalimbali yalitumika kuwaleta mastaa mpaka kwenye stage...
-
Justin Bieber ambaye hivi sasa yuko katika kipindi cha matazamio ameripotiwa kuhatarisha maisha ya watembea kwa miguu katika eneo la Beve...
-
The Rock says his mom, Ata Maivia-Johnson and his cousin were struck HEAD ON by a drunk driver this week ... and luckily, they su...
0 comments:
Post a Comment