Tuesday, August 12, 2014
On 5:21 AM by Unknown No comments
Mitandao ya kijamii inawaleta watu pamoja na kurahisisha mawasiliano, lakini mtandao huu umekuwa sehemu rahisi pia ya watu kulizwa kwa utapeli au usaliti.
Msanii mpya wa Bongo Flava aliyejitambulisha kwa jina la Cyju, Jumatatu wiki hii alifikisha malalamiko yake kupitia kipindi cha The Jump Off cha 100.5 Times Fm kuwa rapper wa Salasala Godzilla amemzulumu pesa yake aliyomlipa kwa ajili ya kufanya nae collabo.
Cyju ameeleza kuwa aliwasiliana na Godzilla Facebook, kwenye ukurasa wa mtu anaejiita ‘Godzillah Golden Kingzilla’ na baadae wakapeana namba za simu ili wakamilishe zoezi huku akimuomba 250,000 kama malipo ya collabo hiyo.
Cyju anasema baada ya mazungumzo marefu kwa njia ya simu jamaa alimpunguzia hadi shilingi 50,000. Na bila hiana jamaa alijichanga na kumtumia mtu huyo huku akimsisitiza kuwa asimuangushe. Lakini siku ya siku jamaa aligeuka na kukata mawasiliano baada ya kupewa mkwanja.
“Eid Pili nikampigia sasa asubuhi. Ikawa inaita simu hapokei..nikapiga tena hapokei. Kumcheck whatsapp kanibroke. Nikaamua kuingia FB nikamuuliza kwa hiyo Zilla ndo umenizingua? ‘Akanijubu hamna mdogo wangu’. Nikamuuliza ‘ila’..hakujibu tena na ndio mpaka hivyo.”
The Jump Off ilimtafuta Godzilla halisi na kumueleza mkasa huo ambapo alieleza kuwa hajawahi kabisa kuwasiliana na Cyju na kwamba ameshapata malalamiko mengi kuhusu huyo Godzilla fake anaechukua pesa za wasanii kwa madai ya kufanya nao collabo.
“Kuna jamaa mmoja anatumia jina langu facebook anajiita ‘Godzillah Golden Kingzilla ’. Anawaibia sana watu, na wengi wameshalalamika sana. Mimi natumia ‘King Zilla From Salasala’ . sasa muulize alikuwa anachat na akauti gani. Halafu muulize mtu aliyekuwa anachat nae kama ana namba kama hii tunayoongea na wewe.” Alisema Godzilla.
Ukweli ni kwamba Cyju alitapeliwa na mtu huyo aliyegeuza jina la rapper Godzilla wa Salasala kuwa kitega uchumi chake. Namba aliyoionesha Cyju sio namba halisi ya rapper huyo.
Shtuka, hakikisha unaewasiliana nae Facebook unamfahamu kabla ya kufanya nae biashara yoyote…hata kuanzisha nae uhusiano
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Slider
MusicView All
TechnologyView All
PicturesView All
GamesView All
Labels
Category
Ads
Text
Find Us On Facebook
Link List
Contact Form
Blogroll
Flickr Images
728x90 AdSpace
Label
FashionView All
Latest News
Popular Posts
-
Tumezoea kusikia wakati wa kufunga ndoa watu wakila kiapo kuwa watapendana hadi kifo kitakapowakuta, kia...
-
Brad Pitt and Angelina Jolie will finally tie the knot, only for a movie. According to a scoop from The Hollywoo...
-
Miley Cyrus updated her Instagram with lots of photoshopped pictures. This time, Justin Bieber 's Calvin Kl...
-
Brad Pitt has owned a gun since he was very young. In a new interview with Radio Times to promote his new flick " Fury ", the a...
-
Will Smith , who is gearing up for his new film " Focus " with Margot Robbie , opens up about his experience in 25 y...
-
Lil Wayne ni msanii wa Hiphop lakini aliwahi kujaribu kutoa album ya rock ambayo inaitwa Rebirth yenye hit singles kama Knock Out na Porm ...
-
Mara nyingi birthday party za washkaji huwa zinasindikizwa na umwagiwaji wa maji kwa mhusika,sasa unaambiwa hii ya Shetta imekua kibok...
-
Channel O walitisha sana na maandalizi ya mwaka huu wa 2014 ambapo magari mbalimbali yalitumika kuwaleta mastaa mpaka kwenye stage...
-
Diamond Platnumz ameingia Dar es salaam usiku wa July 10 mashabiki wengi wakiongozwa na mama yake,dada yake pamoja na mpenzi wake Wema S...
0 comments:
Post a Comment