Monday, October 6, 2014
On 5:55 AM by Unknown No comments
Rapper Noorah aka Babastylez amesema kama isingekuwa neema za Mungu, leo hii asingekuwepo
duniani.Akiongea kwenye kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds TV hivi karibuni, Noorah alidai alikuwa na tatizo la kujikunja kwa utumbo lililodumu kwa miaka 20. Amesema wakati tumbo likimuuma alikuwa akidhani ni vidonda vya tumbo.
“Doctor amekuja kunifanyia operesheni, baada ya operesheni akamuita mama pembeni. Akamwambia ‘mama huyu mwanao ana Mungu sana’. Maana kitu alichokikuta huko tumboni, hakuna binadamu anaweza akawa hai kwa hali ile. Utumbo wangu mdogo ulikuwa umejikunyata wote. Akauliza ‘alikuwa anapataje choo huyo!’
Alisema operesheni hiyo ilidumu kwa masaa sita na ilifanyika kwenye hospitali ya Kairuki jijini Dar es Salaam.
“Nimetoka dokta anasema utumbo wangu ulikuwa umekuwa mdogo kama wa mtoto mchanga kwahiyo ulikuwa unapitisha chakula kwa tabu sana. Kwahiyo kipindi hicho nilikuwa nakula vyakula vya kusaga tu, na vyenyewe sometimes vingine havipiti.”
Pamoja na kuwa amepona tatizo hilo, Noorah amesema ana tatizo jingine linalofanya awe anapata vitu kama vifafa (seizure) ambavyo vimesababisha na ajali aliyopata mwaka 2005 iliyomfanya apate tatizo kwenye ubongo. “Sasa hivi dokta ameshanipa treatment na ameniomba nije nipate mind rest,” alisema Noorah ambaye kwa sasa amerejea kwao Shinyanga kama sehemu ya maagizo ya wataalam.
Noorah aliwaasa wasanii na watu wengine kuwa na desturi ya kuchunguza afya zao mara kwa mara kubaini matatizo yanayowasumbua.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Slider
MusicView All
TechnologyView All
PicturesView All
GamesView All
Labels
Category
Ads
Text
Find Us On Facebook
Link List
Contact Form
Blogroll
Flickr Images
728x90 AdSpace
Label
FashionView All
Latest News
Popular Posts
-
Tumezoea kusikia wakati wa kufunga ndoa watu wakila kiapo kuwa watapendana hadi kifo kitakapowakuta, kia...
-
Nicki Minaj didn't seem to have big problems with hilarious memes appearing on the internet following the release of her...
-
Miley Cyrus updated her Instagram with lots of photoshopped pictures. This time, Justin Bieber 's Calvin Kl...
-
Mr Blue aka Kabayser ameanzisha taasisi ya ‘Micharazo Foundation’ itakayoanza kupokea wasanii wapya na pia itakuwa sehemu ya kukuza vipaj...
-
Lil Wayne ni msanii wa Hiphop lakini aliwahi kujaribu kutoa album ya rock ambayo inaitwa Rebirth yenye hit singles kama Knock Out na Porm ...
-
Kikosi Kazi cha Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya nchini kimemhoji kwa zaidi ya saa 10, msanii Agnes Gerald ‘Masogange’ kuhusiana na tuhum...
-
Yemen imesema wapiganaji wa kundi la al-Qaeda wamewaua watu sita katika mapi...
-
Brad Pitt has owned a gun since he was very young. In a new interview with Radio Times to promote his new flick " Fury ", the a...
-
Mara nyingi birthday party za washkaji huwa zinasindikizwa na umwagiwaji wa maji kwa mhusika,sasa unaambiwa hii ya Shetta imekua kibok...
-
Will Smith , who is gearing up for his new film " Focus " with Margot Robbie , opens up about his experience in 25 y...
0 comments:
Post a Comment