Thursday, November 27, 2014

On 4:07 AM by Unknown   No comments
diamond2
Diamond Platnumz tayari ametua jijini Johannesburg, Afrika Kusini toka jana, tayari kuhudhuria tuzo za Channel O (CHOAMVA) zinazotarajiwa kutolewa siku ya Jumamosi Nov.29 akiwa anawania vipengele vinne.
Staa huyo ambaye ameachia ngoma mpya siku chache zilizopita ‘Ntampata wapi’, ameandika kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamaii kuwa pia leo Alhamisi Nov.27 atapata nafasi ya kuingia kwenye jumba la Big Brother kubadilishana mawazo na washiriki.
“Tafadhali usikose kuangalia Big Brother Afrika kuanzia saa tano Asubuhi kesho (leo), kijana wako Platnumz ntakuwa ndani ya nyumba nikizoza mawili matatu na washiriki….” aliandika

0 comments:

Post a Comment