Monday, December 1, 2014
On 1:40 AM by Unknown No comments
Babalevo amewachokoza nyuki na sasa anauguza maumivu.
Rapper huyo amejikuta akipokea matusi ya kila aina kutoka kwa mashabiki wa Alikiba waliochukizwa na ujumbe wale wa dhihaka kwa mfalme wao, hitmaker wa ‘Mwana’.Pengine akitafuta njia ya kuongeza ucheshi kwenye ujumbe wake wa pongezi kwa Diamond kufuatia ushindi wake kwenye tuzo za Channel O, Jumamosi hii, Babalevo alipost picha ya kitanzi na kuandika:
Ally kiba naomba uingie mwenyewe coz umeyataka mwenyewe.. sungura ulikuwa umesha mkamata eti umemuachia kiboya boya sasa kumkamata tena itaghalimu miaka mitano… Sisi wote Tupo kwenye Sanaa ila nguvu tunazidiana ndomana ally nilikuona mkombozi Wetu coz we ni fundi muziki.. Inakuwa je unajianguaha kwenye kumi na nane?????? Badala ya kufunga unategemea penati… Ona sasa refa kapeta… Na kufanya Kwa sasa tukubali bwana @diamondplatnum ni #KIBOKO japo alikwapua Ka aidia kangu na ndo kanakompa mijituzo.. Ila nime hands up… Ally kiba na diamond wote ni ma home boy kutoka KIGOMA ila mnyonge mnyongeni Haki yake mpeni… Hii ni kick kuna mtu yeyote mwenye snea?”
Ujumbe huo ulisababisha hasira isiyo kifani kutoka kwa mashabiki wa Alikiba ambao kama wangeweza kumuona live muda huo, huenda angechezea kichapo kikali.
“Hv ww unahc unaweza mfkia Aly kiba cku moja kichwa kikubwa akil tope nngekuona wa mana ungechochea kuelewana kwao bt ndo kwanza unaongea pumba kutafta tension au ndo kujpendekeza kwa dai kwa style hyo hv unaelewa unachoimbaga au unafoka tu na ushkuru kigoma oll star ilkutoa wngne tulkua ht hatukujui tulza mshono uctafte kick kwa nguvu,” aliandika mmoja.
“Hahaaaaa anaangaika huyooo maana hata mwanangu nikimuuliza hakujui. Pyeeeeeeeeeee.unaacha kusifia tunzo iliopatikana nikwawantanzania unaanza kutaja majina yawatu.hata Wewe siunaimba kwann jamani kwann umseme mwenzio.jitahidi nawewe boya Wewe,” aliandika mwingine.
Mwigine aliandika: Sura yenyewe imekomaa kama ngozi ya goti mm sijawahi kukuelewa hata cku moja kwenye kazi zako yaani nilishakusahau kama na ww unaimba kama vp rudi kigoma ukavue dagaa kama mziki umekushinda waache watoto kina kiba wenye mji wao mtu mkubea akili huna jipangee.”
Baada ya kuona risasi aliyoipiga imemrudia mwenyewe, Babalevo alijaribu kuweka mambo sawa kwa kupost picha nyingine akiwa na Alikiba na kuandika:
“Ally kiba eeeeeeeeeeeeeeeeee niokoe babaaaaaaaa…… mashabiki wako watanimalizaaaaaaaaaa…. Mi nilikuwa kwenye maswala ya kutoa maoni tu babaaa……coz @diamondplatnumz ametunyooooooshaaaaaa…..sasa we ndo #mkombozi tuliye kuchagua tuokoe babaaaaaaa…… Kachukua tuzo tatu si unajua anatumia nguvu za GIZAAAA?
Hapana chezea mashabiki wa ‘Mwana Dar es Salaam’
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Slider
MusicView All
TechnologyView All
PicturesView All
GamesView All
Labels
Category
Ads
Text
Find Us On Facebook
Link List
Contact Form
Blogroll
Flickr Images
728x90 AdSpace
Label
FashionView All
Latest News
Popular Posts
-
It's good to be Iron Man — Robert Downey Jr. once again leads Fo...
-
Tumezoea kusikia wakati wa kufunga ndoa watu wakila kiapo kuwa watapendana hadi kifo kitakapowakuta, kia...
-
Arnold Schwarzenegger was born and raised in Austria. But The Expendables 3 star looked like a true American as he left Cafe Roma in Beverly...
-
Brad Pitt and Angelina Jolie will finally tie the knot, only for a movie. According to a scoop from The Hollywoo...
-
Lil Wayne ni msanii wa Hiphop lakini aliwahi kujaribu kutoa album ya rock ambayo inaitwa Rebirth yenye hit singles kama Knock Out na Porm ...
-
ITALIA imeaga Kombe la Dunia nchini Brazil baada ya kufungwa 1-0 na Uruguay, bao pekee la Diego Godin katika mchezo ambao mshambuliaji Luis ...
-
Baada ya habari za ndege ya Malaysia airline hivi sasa ajali nyingine imetoka karibu kabisa na Tanzania ambapo ni nchini Uganda. Ndege hiy...
-
Channel O walitisha sana na maandalizi ya mwaka huu wa 2014 ambapo magari mbalimbali yalitumika kuwaleta mastaa mpaka kwenye stage...
-
Mwaka huu Psquare hawataki mchezo na mtuu baada ya kuachia nyimbo tatu kwa mpigo ikiwemo sapraiz ya nguvu ya video yao mpya inayoitwa Ej...
0 comments:
Post a Comment